Dua hiyo imepanga kufanyika Ijumaa, Novemba 4 katika msikiti wa kitaifa huko Accra.
Ibada hiyo itaongozwa na Imamu Mkuu wa Ghana Sheik Osman Nuhu Sharubutu, huku viongozi wa SGFA wakihudhuria.
GFA iliandika: "Kama sehemu ya shughuli zilizopangwa kabla ya Black Stars kushiriki katika Kombe la Dunia la FIFA litakaloandaliwa nchini Qatar, Shirikisho la Soka la Ghana litatembelea msikiti mkuu wa Accra kushika Sala ya Jummah.
"Dua hii maalum itaongozwa na Imamu Mkuu wa Kitaifa, Sheikh Osmanu Nuhu Sharubutu siku ya Ijumaa, Novemba 4, 2022.
"Wajumbe wa baraza kuu, timu ya Ufundi na usimamizi ya Black stars, wafanyakazi wa GFA, makundi mbalimbali ya wafuasi na umma kwa ujumla wote wamealikwa."
Black Stars wanajiandaa kwa Kombe la Dunia, litakaloanza Qatar mnamo Novemba 20.
Ghana wamepangwa Kundi H pamoja na Ureno, Korea Kusini na Uruguay.
Ghana ni nchi iliyoko Afrika Magharibi. Uislamu ni dini ya pili kwa wafuasi wengi nchini humo baada ya Ukristo.
3481093