IQNA

Utawala wa Kizayuni washadidisha jinai dhidi ya Wapalestina

15:20 - May 07, 2016
Habari ID: 3470299
Jamii ya kimataifa imeingiwa na wasiwasi kutokana na kushahidi jinai za utawala wa Kizayuni Israel dhidi ya Wapalestina.
Kuhusiana na suala hili, Idara ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Palestina OCHA siku ya Ijumaa ilitoa taarifa na kukosoa vikali kuenea jinai za Israel dhidi ya Wapalestina na kubaini kuwa katika kipindi cha wiki moja iliyopita, wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wamewaua shahidi Wapalestina kadhaa na kuwajeruhi wengine 85. Aidha katika kipindi cha wiki moja sasa wanajeshi wa Israel wamehujumu na kubomoa makumu ya nyuma za Wapalestina.
Kwa mujibu wa ripoti ya OCHA, kwa kisingizio cha kutafuta njia za chini ya ardhi zinazotumiwa na Hamas katika eneo la mapaka wa Ghaza na Misri, katika kipindi cha siku nne zilizopita, jeshi la Israel limetekeleza mashambulizi makubwa katika eneo hilo. Siku ya Ijumaa eneo la Khan Yunis mashariki mwa Ghaza lilishuhudia mashambulizi ya kuogofya ya Utawala wa Kizayuni ambalo Wapalestina kadhaa waliuawa shahidi au kujeruhiwa.
Matukio ya wiki moja iliyopita Palestina yanaashiria kushadidi ukandamizaji wa utawala wa Kizayuni na kueneza sera za kujitanua za utawala huo.
Ni kwazi kuwa, kwa jinai zake hizo, utawala wa Kizayuni unatafuta fursa ya kueneza sera zake za kujitanua, uporoaji ardhi, na kuwakamdamiza wapigania ukombozi wa Palestina. Utawala huo unatumia nguvu za kijeshi kufikia malengo yake haramu.
Kuedelea ukandamizaji na ukatili wa utawala wa Kizayuni dhidi ya watui waiso na ulinzi wa Palestina ni ukiukwaji wa wazi wa mikataba ya kimataifa ya Geneva. Hivi sasa walimwengu wanafahamu jinai dhidi ya binadamu za utawala wa Kizayuni na suala ambalo imepelekea kuwepo malalamiko dhidi ya utawala huo dhalimu wa Israel.
Hii ni katika hali ambayo ripoti za kimataifa dhidi ya Israel hazifuatiliwi katika Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa kutokana na vizingiti vinavyowekwa na Marekani na baadhi ya nchi za Magharibi katika baraza. Himaya hiyo ya Marekani imepelekea utawala wa Kizayuni upate kiburi zaidi kutekeleza jinai zake.
Pamoja na kushahidi jinai za utawala wa Kizayuni kumepelekea hali ya Wapalestina kuwa mbaya, lakini ukandamizaji huo haujawafanya Wapalestina wasalimu amri mbele na utawala wa Kizayuni.
Watu wa Palestina kwa kutegemea mapambano yao dhidi ya Uzayuni, wamesisitiza kuendelea kusimama kidete mbele ya utawala wa Kizayuni na kupelekea utawala huo kufeli katika njama zake, na hata wakuu wa Israel wamekiri hilo.
Kuhusiana na maudhui hii, mkaguzi mkuu wa Utawala wa Kizayuni amekosoa utendaji kazi wa waziri mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu katika hujuma yake ya siku 50 dhidi ya ukanda wa Ghaza mwezi Juni mwaka 2014.
Yosef Shapira Mkaguzi Mkuu wa Israel katika ripoti yake kuhusu utendaji kazi wa baraza la mawaziri la Israel katika vita hivyo vya siku 50 dhidi ya ghaza amesema, "utendaji wa Netanhayu katika vita hivyo ulikuwa dhaifu na vita hivyo vilimalizika wka hasara ya Israel."
Kanali ya pili ya televisheni ya utawala wa Kizayuni imesema ripoti hiyo kuhusu vita vya siku 50 vya Ghaza ni bomu katika siasa za utawala huo na kwamba ripoti hiyo ikitangazwa hadaharani basi kutaibuka mgogoro mkubwa.
Utawala wa Kizayuni unaendeleza hujuma zake dhidi ya Ghaza katika hali ambayo hujuma hizo si tu kuwa hazijafikia malengo yaliyoainishwa bali pia zimepelekea kufeli zaidi utawala huo ghasibu na hivyo kupelekea kuiubuka mifarakano zaidi ndani ya utawala huo.
Katika hali kama hii, utawala wa Kizayuni umeanzisha duru mpya ya hujuma dhidi ya ukanda wa Ghaza ili kujaribu kufunika kufeli kwale na pia kupotosha fikra za umma ndani ya utawala huo.
Lakini matukio ya Palestina yanaashiria kuwa chokochoko mpya za utawala wa Kizayuni Ghaza hazitakuwa na natija nyingine ghairi ya kutumbukia utawala huo katika kinamasi cha kujitakia wenyewe.
3459732
captcha