Tukio hilo lilijiri saa nne usiku Alhamisi karibu na msikiti wa Darul Farooq. Kiongozi huyo wa Waislamu aliyelengwa ametajwa kuwa Sheikh Mohamed Mukhtar mwenye umri wa miaka 50. Mkurugenzi wa Msikiti wa Darul Farooq amesema Waislamu daima wanaishi katika hofu ya kuhujumiwa.
Kufuatia tukio hilo, Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani, CAIR, Tawi la Minnesota limetaka wakuu wa jimbo hilo wafanya uchunguzi kamili kuhusu hujuma hiyo.
Tukio hilo limejiri kairbuni miaka mitatu baada ya msikiti huo kuhujumiwa na kuharibiwa vibaya.