Maandamano ya kupinga vita vya Israel kwenye Ukanda wa Gaza yamekuwa yakiwavutia maelfu ya watu nchini Morocco tangu mzozo huo uanze zaidi ya miezi miwili iliyopita.
Maandamano ya Jumapili yaliratibiwa kwa pamoja na vikundi vya mrengo wa kushoto na kundi lililopigwa marufuku lakini lililovumiliwa na Al-Adl Wal-Ihsan.
Waandamanaji walipeperusha bendera za Palestina na kushikilia mabango yaliyoandikwa "mapambano (muqawama) hadi ushindi," "komesha uhusiano wa serikali ya Morocco na Israel" na "Palestina huru."
Morocco ilikubali kurejesha uhusiano na Israel mwaka 2020, chini ya shinikizo kutoka kwa serikali ya Marekani.
Waandamanaji katika maandamano ya Jumapili pia walitoa wito wa kususia bidhaa za mashirika yanayohusiana au yanayounga mkono Israel.