Mbali na Sha’ban na Ramadhani, mwezi wa Rajab una fahari kubwa, kama ilivyotajwa katika riwaya nyingi ambazo pia zimefafanua sifa za mwezi huu.
Imepokewa kutoka kwa Mtukufu Mtume Muhammad (SAW) akisema: “Iwapo mtu atafunga siku moja ya mwezi wa Rajab, bila shaka atapata Radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu, ataondolewa kwenye ghadhabu yake, na milango ya Moto itaondolewa usoni mwake.”
Hapa kuna baadhi ya Aamal (amali njema na ibada) zilizopendekezwa katika mwezi wa Rajab:
- Astaghfiru Allah wa asaluhu alttawbata
Ninamuomba Mwenyezi Mungu msamaha na ninamuomba akubali toba yangu.
Subhana al-ilahi aljalili
Utukufu ni wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Subhana man la yanbaghi alttasbihu illa lahu
Ametakasika Ambaye hatakiwi kutukuzwa ghairi yake
Subhana al-a`azzi al-akrami
Utukufu ni wa Mwenye utukufu na hishima
Subhana man labisa al`izza wa huwa lahu ahlun
Ametakasika ambaye amejivika utukufu usiomfaa yeyote ila Yeye.
Astaghfirullaha alladhy la ilaha illa huwa
Naomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu. Hapana mungu ila Yeye,
Mmoja wa pekee ambaye hana mshirika.
wa atubu ilayhi.
na ninatubu mbele yake.
La ilaha illa allah
Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu.
Astaghfirullaha wa atubu ilayhi
Naomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na ninatubu kwake.
Baada ya hayo kurudia mara sabini, inua mikono kuelekea mbinguni na useme:
Allahuma aghfir li wa tub’alayya
Ewe Mwenyezi Mungu, (tafadhali) nisamehe na ukubali toba yangu.
Astaghfiru Allaha dhaljalali wal ikrami
Namuomba Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa utukufu na utukufu.
Min jami i aldhunubi wa ithmi
kunisamehe dhambi na makosa yangu yote.
Mwenye kusoma Surah Tawhid mara 100 siku ya Ijumaa katika Rajab atafurahia, Siku ya Kiyama, nuru inayomvuta kuelekea Peponi.
Swala maalumu siku Ijumaa katika Rajab -Iqbal Aamal
Yafuatayo yanapatikana kupitia mlolongo wa nyaraka kutoka kwa Abdullah ibn Abbas, kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW): “Swali rakaa nne za sala baina ya Adhuhuri na Sala ya Alasiri siku ya Ijumaa katika mwezi wa Rajab na katika kila rakaa ya swala soma Surah Al-Fatiha mara moja, Ayat al-Kursi mara saba, “Surah Al-Ikhlas” mara tano, kisha baada ya hapo sema mara kumi dhkri ifuatayo:
Astaghfiru allaha wa as’aluhu altawbata
Ninamuomba Mwenyezi Mungu msamaha na ninamuomba anikubalie toba yangu.