IQNA

Mwezi wa Ramadhani

Dua za Kila Siku za Mwezi wa Ramadhani- Siku ya 17

Dua hizi za kila siku za Mwezi wa Ramadhani husomwa toka mwanzo ya tarehe mosi Ramadhani hadi siku ya mwisho katika mwezi huu mtukufu. Kila dua ina siku yake, na inaweza kusomwa mara nyingi kadiri ya uwezo wa mtu mwenyewe.

Ee Mwenyezi Mungu! Niongoze katika mwezi huu kwenye amali njema, Unitekelezee katika mwezi huu haja zangu na mataraji yangu, Ewe Usiyehitaji ufasiri na kuuliza (ndipo ukaifahamu haja ya mja, bali Unaifahamu hata bila ya kuuliza na bila kuelezwa). Ewe Mjuzi wa yalioyomo vifuani (nyoyoni) mwa walimwengu! Mteremshie rehema na amani (Mtume) Mohammad (s.a.w.) na Aali zake watakatifu.

Kishikizo: dua za kila siku ، ramadhani